Search

Saturday, January 21, 2012

MISA-Tanzania urges citizens to lobby for Access to Information during election campaigns

MISA-Tanzania has urged citizens to ask candidates vying for various political posts during the coming general election on how they are going to promote access to information in the country, including lobbying the government to enact the long awaited Right to Information law. 

Tuesday, June 01, 2010

The ROLE OF MEDIA in the agricultural...

INFORMATION, RESOURCES, MULTIDISCIPLINARY AND MEDIA ENVIRONMENT FOR AGRICULTURAL DEVELOPMENT IN TANZANIA - A poster  presented in CTA Annual Seminar - THE ROLE OF MEDIA in the agricultural and rural development of ACP Countries in Brussels, Belgium 12-16 October, 2009.
The media houses in Tanzania lack information resources such as libraries, internet connectivity, information collection, and well trained staff to serve and meet journalistic desires and needs. This also includes the issue of multidisciplinary media staff in the area of agriculture and its allied fields. With a multidisciplinary component among media practitioners, the current move by policy-makers in Tanzania, Africa and the world in general to make agriculture a number one priority can be achieved successfully if the media play a major role.


Tuesday, January 30, 2007

Nini maana ya kuwa msomi na mtaalamu wa fani husika?

Nini maana ya kuwa mhitimu katika fani au sekta husika? Je Watanzania wasomi tunaelewa maana halisi ya kujishughulisha na fani/utaalamu fulani au kusomea fani hizo kama ijulikanavyo na wengi wa wanafunzi katika Vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu hapa nchini? Ionekanavyo ni bado hatujaweza kuzitumia fani/taaluma hizo kwa maendeleo ya nchi yetu, Je tatizo liko wapi na ni kwanini basi kuwepo na hali hiyo? Fuatilia makala hii ili tusaidiane mawazo katika kueleweshana na kujaribu kupata ufumbuzi wa tatizo hili ndani ya jamii ya watanzania.

Ni wangapi walioko katika fani mbalimbali hapa nchini wanaweza kujivuna kuwa wamechangia kwa kiwango cha kupigiwa mfano au hata kiwango cha chini kabisa katika fani zao? Kama ni kuwataja basi itakuwa ni wachache sana ikilinganishwa na idadi ya waliosomea fani/taaluma hizo husika. (Najua sio wengi kama ipasavyo kuwa). Ni katika siasa tu ambako kwa matazamo wangu kuna mengi lakini mimi sitazungumzia huko. Sina maana kuwa sithamini mchango wa wanasiasa, la hasha ila katika makala hii sikusudii kuangalia masuala ya wanasiasa.


Sunday, January 14, 2007

Uwajibikaji uko wapi kwa viongozi wetu?
Nini maana ya kuwa kiongozi wa umma? Je wengi wa viongozi wetu wanaelewa dhana hii nzima ya kuutumikia umma au jamii? Je walioko madarakani na wanaoongozwa wanaonyesha na kufahamu wajibu wao kwa jamii na kuwa viongozi bora wa kuigwa na kizazi chetu cha baadae? Haya ni baadhi ya maswali ambayo nitajaribu kuyaongelea katika makala yangu hii.

Kwa Tanzania ni dhahiri kuwa moja kwa moja wengi wa viongozi walioko madarakani katika sehemu mbali mbali mbali serikalini na katika taasisi mbalimbali wameshindwa kuwa ni mfano bora wa mtu mwadilifu anayeongoza jamii anavyopaswa kuwa. Wamekuwa ving’ang’anizi wa madaraka na kusahau kuwa umma unawaangalia na katika umma huu kuna watu wa silka, umri na uwezo mbalimbali wa kuchambua mambo katika jamii.
Dhana ya Ujasiriamali na utendaji wa viongozi Tanzania
Nitazungumzia dhana ya ujasiriamali na utendaji wa viongozi wetu na mazingira yao katika taasisi na sekta mbalimbali kwa ujumla hapa Tanzania. Kwani mengi ya matatizo ambayo tunakumbana nayo sasa hivi katika maisha, uendeshaji na utekelezaji wa kazi kila siku kwa matazamo wangu ni kutokana na viongozi hao kukosa au kutoelewa maana halisi ya ujasiriamali.

Hivi sasa wengi tumeichukulia na kuihusisha dhana hii na upande wa biashara tu, jambo ambalo ni kosa kubwa tunalolifanya na inawezekana ikawa ndio sababu ya kuwa na matatizo lukuki ndani ya jamii bila ya kuwa na suluhisho nayo kwa sababu viongozi tulionao hawana au hawaelewi dhana nzima ya ujasiriamali.
Nafasi ya vyombo vya habari na utendaji wake
Nitagusia kwa uchache juu ya uhuru wa kueleza na kupata habari ikiwemo kile kinacholetwa kwa jamii toka katika vyombo vya habari kupitia waandishi, watunzi na wapigapicha na zaidi nitaangalia jukumu lililopo kwa wenye fani hizo pamoja na vyombo vyao katika kuhakikisha kuwa utamaduni, utu, silka na maadili yanazingatiwa bila ya kukiuka suala la msingi la haki za binaadamu.

Hapa Tanzania hadi mwishoni mwa miaka ya themanini kulikuwa na magazeti na vyombo vichache vya habari na vyote vilikuwa vinamilikiwa na Taasisi za Serikali, hivyo habari zake zaidi ziligusia siasa na maendeleo ya nchi zaidi kuliko habari nyingine za burudani na matukio mengine ye kawaida na hata hizo za burudani zilizotolewa zilikuwa zinazingatia maadili na heshima ya jamii yetu.
Tangazo la condom na utamaduni wa Mtanzania
Uamuzi wa kukataa jambo ni wa mtu binafsi ingawa mazingira nayo yanachangia kwa kiasi kikubwa juu ya uamuzi huo. Kweli tuko katika dunia huru – dunia kijiji kimoja, lakini mazingira ya nchi moja na nyingine ni tofauti kutokana na utamaduni na silka za watu wake. Jambo lifanywalo na nchi moja isiwe ni sababu ya kufanywa au kufuatwa na nchi nyingine kwa sababu ya utandawazi, naamini uhuru wa kuamua kufuata au kutofuata bado tunao hatujanyang’anywa uhuru huo.

Nasema haya kwa sababu sasa hivi wananchi tunanyang’anywa uhuru wetu kwa nguvu zote kutokana na nguvu walizonazo wamiliki wa vyombo vya habari. Kwanini? Nitazungumzia tangazo la kondomu aina ya Salama (Studded) “zenye vipele”. Hilo tangazo sio siri naamini wengi wetu linatunyima uhuru wetu ndani ya nyumba zetu tukiwa na familia zetu.

At class - MUM

At class - MUM
Mazoezi ya uhariri wa picha kwa kutumia kompyuta Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro - MUM

Mjadala studio

Mjadala studio
Wanafunzi wa shahada ya kwanza mawasiliano kwa umma mazoezini studio za Muslim University of Morogoro