Dhana ya Ujasiriamali na utendaji wa viongozi Tanzania
Nitazungumzia dhana ya ujasiriamali na utendaji wa viongozi wetu na mazingira yao katika taasisi na sekta mbalimbali kwa ujumla hapa Tanzania. Kwani mengi ya matatizo ambayo tunakumbana nayo sasa hivi katika maisha, uendeshaji na utekelezaji wa kazi kila siku kwa matazamo wangu ni kutokana na viongozi hao kukosa au kutoelewa maana halisi ya ujasiriamali.
Hivi sasa wengi tumeichukulia na kuihusisha dhana hii na upande wa biashara tu, jambo ambalo ni kosa kubwa tunalolifanya na inawezekana ikawa ndio sababu ya kuwa na matatizo lukuki ndani ya jamii bila ya kuwa na suluhisho nayo kwa sababu viongozi tulionao hawana au hawaelewi dhana nzima ya ujasiriamali.
Hivi sasa wengi tumeichukulia na kuihusisha dhana hii na upande wa biashara tu, jambo ambalo ni kosa kubwa tunalolifanya na inawezekana ikawa ndio sababu ya kuwa na matatizo lukuki ndani ya jamii bila ya kuwa na suluhisho nayo kwa sababu viongozi tulionao hawana au hawaelewi dhana nzima ya ujasiriamali.