Nafasi ya vyombo vya habari na utendaji wake
Nitagusia kwa uchache juu ya uhuru wa kueleza na kupata habari ikiwemo kile kinacholetwa kwa jamii toka katika vyombo vya habari kupitia waandishi, watunzi na wapigapicha na zaidi nitaangalia jukumu lililopo kwa wenye fani hizo pamoja na vyombo vyao katika kuhakikisha kuwa utamaduni, utu, silka na maadili yanazingatiwa bila ya kukiuka suala la msingi la haki za binaadamu.
Hapa Tanzania hadi mwishoni mwa miaka ya themanini kulikuwa na magazeti na vyombo vichache vya habari na vyote vilikuwa vinamilikiwa na Taasisi za Serikali, hivyo habari zake zaidi ziligusia siasa na maendeleo ya nchi zaidi kuliko habari nyingine za burudani na matukio mengine ye kawaida na hata hizo za burudani zilizotolewa zilikuwa zinazingatia maadili na heshima ya jamii yetu.
Hapa Tanzania hadi mwishoni mwa miaka ya themanini kulikuwa na magazeti na vyombo vichache vya habari na vyote vilikuwa vinamilikiwa na Taasisi za Serikali, hivyo habari zake zaidi ziligusia siasa na maendeleo ya nchi zaidi kuliko habari nyingine za burudani na matukio mengine ye kawaida na hata hizo za burudani zilizotolewa zilikuwa zinazingatia maadili na heshima ya jamii yetu.