Tangazo la condom na utamaduni wa Mtanzania
Uamuzi wa kukataa jambo ni wa mtu binafsi ingawa mazingira nayo yanachangia kwa kiasi kikubwa juu ya uamuzi huo. Kweli tuko katika dunia huru – dunia kijiji kimoja, lakini mazingira ya nchi moja na nyingine ni tofauti kutokana na utamaduni na silka za watu wake. Jambo lifanywalo na nchi moja isiwe ni sababu ya kufanywa au kufuatwa na nchi nyingine kwa sababu ya utandawazi, naamini uhuru wa kuamua kufuata au kutofuata bado tunao hatujanyang’anywa uhuru huo.
Nasema haya kwa sababu sasa hivi wananchi tunanyang’anywa uhuru wetu kwa nguvu zote kutokana na nguvu walizonazo wamiliki wa vyombo vya habari. Kwanini? Nitazungumzia tangazo la kondomu aina ya Salama (Studded) “zenye vipele”. Hilo tangazo sio siri naamini wengi wetu linatunyima uhuru wetu ndani ya nyumba zetu tukiwa na familia zetu.
Nasema haya kwa sababu sasa hivi wananchi tunanyang’anywa uhuru wetu kwa nguvu zote kutokana na nguvu walizonazo wamiliki wa vyombo vya habari. Kwanini? Nitazungumzia tangazo la kondomu aina ya Salama (Studded) “zenye vipele”. Hilo tangazo sio siri naamini wengi wetu linatunyima uhuru wetu ndani ya nyumba zetu tukiwa na familia zetu.